Language: Swahili
Publication Year: 2015
Sisi katika Muungano wa sayansi ni azimio letu
kwamba miaka kumi na tano kutoka sasa bioteknolojia za kilimo zinazokuzwa
na wanasayansi wa sekta ya umma
zitaleta maendeleo katika maisha ya watu duniani.
Miaka kumi na tano kutoka sasa wakulima wote duniani watapanda mimea ambayo
inahitaji dawa chache za wadudu wa mimea na viongezi vya kemikali.
Nao mchele ndizi na mihogo iliyoimarishwa kibiolojia
itaboresha lishe kwa mabilioni ya watu.
Mbiringanya na kunde zenye BT zitapunguza matumizi ya dawa za wadudu wa mimea
hivyo basi kunufaisha wakulima, watumizi wa mazao na mazingira.
Mimea nayo itastawi katika hali ya hewa isiyotabirika
kwa hivyo kuhimili joto ukame wadudu na magonjwa
na pia kuweza kutumia kwa ufanisi zaidi
rasilimali chache kama nitrojeni na maji.
Sisi katika Muungano wa sayansi ni azimio letu
kwamba katika miaka kumi na tano kutoka sasa watu kutoka kila sehemu
watakuwa wameweza kutumia mbinu bunifu
ambazo zitaboresha mazingira, usalama wa chakula
na pia maisha duniani.
Narrated by: Angela Siele
Special thanks: Tom Mbega
GMO , Bt
AfS , Food Security
Agricultural Biotechnology , Agriculture , Science Communication
Biotechnology, Insects, Pesticides, Food security, Farmers
26 Jan 2015
131 Views
0 Downloads
0 Rating by People
No comment yet.